Natamba
nami sishibi, wanoshiba hawatambi,
Napamba
mimi shababi, baba hawabebi tambi,
Naamba
sina hababi, Habiba ana vitimbi.
Nawaka
mimi sioki, wanooka sio sisi,
Nasaka
mimi sichoki, wanochoka si wasasi,
Nataka
mimi simaki, wanomaka si asasi,
Nashika
nami sidaki, wanodaka huakisi.
Naita mimi sisiti, wanosita wameketi,
Nakita
mimi sikiti, wasokita ni maiti,
Napita
mimi siwati, wanowata wenyeviti,
Nakata
mimi sifwati, wanofwata mapingiti.
Nikilemewa
si kitu, wasolemewa si watu,
Nikiishiwa
na kitu, wasoishiwa majitu,
Nikipatiwa
si kutu, wasopatiwa vijitu,
Nikipishiwa
na mtu, wasopishwa ni msitu.
Naomba
mimi Yarabi, wanoiba sakubimbi,
Nachimba
mimi sizibi, wanoyaziba mafumbi,
Nabamba
mimi si bibi, wanoshiba kumbikumbi,
Nakumba
mimi sibebi, wanaobeba vimbimbi.
Naona
mimi moyoni, kiona una maoni,
Nabana
mimi sineni, kinena unafitini,
Nasana
mimi mbioni, kituna una milioni,
Narina
mimi zingani, kijana una uneni?
©
Tabu Bin Tabu 2012